Thursday, January 31, 2013

KWA TAARIFA YAKO: ZAWADI MACHIBYA MTANGAZAJI NYOTA ALIYEWEKA REKODI NCHINI



Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu.


Zawadi Machibya akiuliza swali kwa waziri mkuu mh. Mizengo Pinda (hayupo pichani) alipotembelea nchini Uingereza mwaka jana.

Katika KWA TAARIFA YAKO hii leo tuko na mtangazaji maarufu nchini na ukanda wa Afrika mashariki . Huyu si mwingine bali ni Zawadi Machibya, mtangazaji wa Shirika la utangazaji la Uingereza BBC tokea mwaka 2009 mpaka hivi sasa (vijana wa sasa wanasema Jembe), akisikika kupitia idhaa ya Kiswahili ya shirika hilo. Awali alikuwa mwajiriwa wa Shirika la utangazaji Tanzania toka mwaka 1994 hadi 2000 akianzia Radio Tanzania, enzi hizo ikiitwa (RTD), kisha kuanzia mwaka 2000 hadi 2008 kwenye runinga ikiitwa TVT, kabla haijabadilishwa kuwa TBC ambako amefanya vipindi mbalimbali kama vya Mahojiano, Tuambie, mijadala, vipindi vya wanawake na watoto, Bunge, vipindi vingine vikiwemo kuripoti matukio, kuandika makala na kadhalika.


Milton na Gift watoto wa Zawadi katika pozi.

Zawadi, mama wa familia ya watoto watatu, Milton, Gift na Godson ana mengi ambayo jamii haiyajui labda kwa watu wake wa karibu. sasa KWA TAARIFA YAKO Zawadi ndiye aliyeweka rekodi nchini kwa kuwa Rais wa kwanza mwanamke katika serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu nchini akiwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza (SAUT) Pia ni mmoja wa waanzilishi wa umoja wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu (TAHLISO). Licha ya hayo, Zawadi ameokoka na anampenda Yesu, akiwa pia amefanya huduma mbalimbali vijijini kabla ya kuingia ulimwengu wa habari, lakini ilikuwaje mpaka akaamua kuingia kwenye media?

"Niliipenda kazi hii tangu mtoto. Nilipenda lugha hata kusomea masomo ya (HGL), na kuwapasha watu habari, matukio, kuwapa taarifa. Nimemaliza shule, JKT( ambako akiwa mafunzoni alikuwa mchungaji akisaidiana na mwenzake anayefahamika kwa jina la Busara).Halafu nikaanza kazi ya Injili vijijini (Singida) semina, mikutano ya nje uimbaji (Huduma Band na akina Pastor Abel Orgenes, Grace Msusu, Magreth, Elia Kisigila, Elisante,Arthur na wengine.) Muda umefika natakiwa chuo, lakini naona tangazo la kazi Daily News-kwa Radio Tanzania, SHIHATA, Idara ya Habari Maelezo. Nika-apply lakini kwakuifanyia maombi mazito barua yangu ya kuombea kazi, nikaziombea barua, nikazituma. Halafu nikaendelea na huduma, wakati Fernandus Venon na huduma ya SOM-School of Ministry ya Morris Cerullo, wakija Singida, nikafanya kazi. Baadaye napokea barua ya kuitwa kwenye usaili na kisha kupata kazi radio Tanzania nikiwa MADHABAHUNI" amebainisha Zawadi.


Watoto wa zawadi, Gift pamoja na Godson.

Lakini vipi kuhusu wokovu na kazi yake anasemaje ''Inatangulia IMANI, ndiyo inanifanya hivi nilivyo. Kuna mamlaka iliyo kuu, ambayo inasimamia na kuongoza kila ninachofanya. Naamini uzima unaanzia rohoni, halafu unashuka kwenye nafsi halafu mwilini. Kama roho haina uongozi HASA WA KIMUNGU, ni vigumu kuvuka majaribu, changamoto, majukumu, na ufahamu -(Knowledge) Chanzo ni kumcha Mungu). Pili, macho ya rohoni. Giza duniani kubwa bila msaada wa macho ya rohoni, si rahisi kuona''.


Zawadi akimwelekeza kitu bwana Julius Malema mwanasiasa kijana maarufu wa Afrika ya kusini alipofika ofisi za BBC London mapema mwaka jana.

"Utakumbuka kuwa Yesu aliwaonya watu juu ya ‘kuwa macho na waandishi wa habari na …..wengineo.’ La msingi ni kuwa uandishi na utangazaji ni kazi ya watu. Unawapa nini, unatangaza nini na je WEWE UNAJUA NINI KUHUSU WATU NA MAISHA YAO KISIASA, KIJAMII, KIUCHUMI, KIMAISHA, UTAMADUNI WAO, IMANI ZAO, n.k.Na unapofika ngazi ya kimataifa kama hivi hii ya BBC, wigo wako kiuelewa lazima uendane na hadhi ya chombo unachokitumikia. Mfano kujua nani anafanya nini wakati gani, kwa manufaa ya nani na kwa kiwango gani na mengine mengi! Hapa utaleta mataifa makubwa ya Ulaya, Marekani, China, Afrika kama Bara, viongozi wake na bila kusahau majanga yanayoikumba dunia likiwemo ‘kudorora kwa uchumi na mzozo kuhusu sarafu ya Euro’ utaona kuwa maeneo mengine kama yanaoendelea huko Australia, hali ikoje na mengine". amesema Zawadi.

KWA TAARIFA YAKO kuna watu mbalimbali ambao wamechangia mafanikio yake katika ulimwengu wa habari, ambapo ameiambia GK kuwa ''Kwa upande wa kazi, ni mzoefu na mwalimu mzuri. Niko kwenye taaluma hii kwa karibu miaka ishirini sasa. Watu wa muhimu kuwakumbuka hapa ni Mama Edda Sanga ndiye aliyenifundisha kazi (RTD), lakini na wengine wazoefu wakiwemo.

Unaweza kumsikia Zawadi vyema kupitia vipindi vya Dira ya dunia, Leo Afrika na vinginevyo kupitia Idhaa ya Kiswahili ya BBC ikikutangazia moja kwa moja kutoka jijini London nchini Uingereza. Zawadi anayo mengi ya kueleza, GK itamtafuta tena kwa maongezi zaidi.


Zawadi Machibya pamoja na John Solombi (ndani ya studio) wakiwa katika moja ya studio zilizokuwa katika jengo la zamani la BBC, Bush House jijini London, hapa ni kipindi cha ''Dira ya dunia''

Zawadi mkono wa kushoto akiwa na John Solombi katika Dira ya dunia.

Zawadi akiwajibika kumtumikia Mungu katika moja ya mikutano vijijini.


Zawadi enzi hizo akiwa katika huduma moja ya kijiji mkoani Morogoro.


Zawadi akiwa pamoja na mumewe Apostle Machibya. picha ya enzi hizo.

Haya mdau wetu hiyo ni ''KWA TAARIFA YAKO'' hii leo kama ulikuwa hujui, vinginevyo tukutane wiki ijayo au wasiliana nasi kwa barua pepe gospelkitaa@post.com. BARIKIWA

Friday, January 4, 2013

IBADA YA KUMUAGA MWANAHABARI FREDDY MTOI LONDON YAGEUKA WASIFU WA MAISHA YAKE

“Alikua mfano dhahiri wa neno mtanashati”
-Zawadi Machibya wa BBC Swahili
Coffin bearers file past-2
Jeneza likitolewa kanisani baada ya ibada.
Kanisa la St Annes Lutheran katikati ya jiji la London juzi Jumamosi lilikuwa kituo maalum cha kumwaga na kuwa wasifu wa maisha ya marehemu Freddy Alex Mtoi aliyekuwa mtangazaji wa BBC Swahili kwa miaka mingi.
Ibada hiyo iliyoendeshwa na wachungaji Tumaini Kalaghe na Mathew Jutta, ilihudhuriwa na wanahabari mbalimbali kutoka BBC , Ofisa wa Ubalozi wa Tanzania, Clement Kiondo, marafiki wa karibu waliomjua marehemu na wanananchi wa sehemu toka Tanzania, Afrika na Ulaya.
Church entrance-built in 1680
Mratibu wa mazishi , Zawadi Machibya, ambaye ni mtangazaji wa BBC, aliendesha shughuli na kuwajulisha wasemaji wote waliozungumzia kwa kuanza kueleza namna neno “mtanashati” lilivyomvaa na kumfaa Freddy Mtoi aliyefariki usiku wa kuamkia Jumamosi tarehe 17 Novemba, 2012.
St Annes Church-notice board-1
Mchungaji Mathew Jutta alikumbusha kwamba safari yetu wanadamu huanzia kwa Mungu na kuishia kwa Mungu. Akailinganisha nsafari hiyo na ile ya kutoka nyumbani Afrika kuja Majuu (palipoitwa Mtoni enzi mchungaji alipokuja Ulaya takribani miaka 20 iliyopita). “Kwa wanaobakia ni huzuni lakini kwa anayesafiri ni furaha yenye matumaini.” Akimzungumzia marehemu alitaka zaidi kututuliza roho tuliyobakia.
Coffin-Mourners show last respect
Kutoa heshima za mwisho
Maneno haya yalisimama dede kama kijiti cha dhamira kuu ya msiba. Kwamba badala ya kuhuzunika tujiratayarishe tunakokwenda kwa kuzingatia maneno ya Biblia, Yohana Mtakatifu 3:20 : “ Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.”
Coffin- females sing past
Maombolezo yakiongozwa na kina dada waliokuwa wakiimba kwa nguvu na hamasa.
Wafanyakazi wenzake marehemu Mtoi nao waliendeleza hoja kwa kutueleza undani wa bidii yake marehemu kazini, tabia yake ya uungwana na upole. Akifafanua kwa kina, mtangazaji wa BBC toka Kenya Solomon Mugera alitoa mfano namna marehemu alipokuwa tayari kumenyeka hata wakati wenzake wakitaka kupumzika kama wakati wa sikukuu ya Krismasi. Mugera :“ Marehemu hakuwa mlalamishi au mbishi. Hakuogopa kujaribu kufanya kitu ambacho hakifahamu.”
Freddy Mtoi- Model pic by Seif Kabelele blog
Marehemu. Enzi zake, aling’ara…na ataendelea kung’aara.
(more…)
Read Full Post »
Idhaa ya Kiswahili ya BBC London inawaarifu wapenzi wa BBC, ndugu, jamaa na marafiki hasa walioko Uingereza kuwa, ibada ya kumuaga mtangazaji wake Fred Mtoi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Jumamosi tarehe 17 Novemba 2012 itakuwa Jumamosi tarehe Mosi Disemba 2012.
Ibada hiyo itafanyika katika Kanisa la St. Anne’s Lutheran mjini London kuanzia saa tano kamili asubuhi.
Anuani ya Kanisa ni: St Anne’s Lutheran Church, Gresham Street, London, EC2V.


Marehem anaongelewa vizuri sana na kila aliyemjua au aliyemsikia akitangaza redioni
Safari ya kuupeleka mwili wa marehemu Dar es salaam nchini Tanzania itakuwa Jumatatu tarehe 3 Disemba 2012 jioni kwa ndege ya Shirika la British Airways.
Mwili unatarajiwa kuwasili Dar es Salaam Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jumanne saa moja asubuhi.
Mipango ya Ibada na mazishi nchini Tanzania inafanyika nyumbani kwa wazazi wake Tabata Maduka Manne jijini Dar es salaam. Ibada ya kumuaga Fred itafanyika katika kanisa la Lutheran Tabata Kuu saa saba mchana siku ya Jumatano tarehe 5 Disemba 2012. Maziko yatafanyika katika makaburi ya Kinondoni Dar es salaam saa tisa alasiri.
Fred alianza kazi ya utangazaji Radio Tanzania kabla ya kuja Ulaya kwa masomo. Amekuwa akifanya kazi huku akiendelea na masomo ya shahada ya pili ya Uzamili kuhusu ‘Digital Media’ katika chuo kikuu kimoja cha London.
Alishiriki katika vipindi muhimu na vilivyopata sifa hasa vya sanaa, utamaduni na jamii kutokana na kuwafahamu wakaazi wengi wa London hasa wenye asili ya Afrika Mashariki.


Marehemu Freddy Mtoi (kulia) akimhoji mwanamuziki Temba mwaka jana alipoitembelea Uingereza- picha na Urban Pulse

Alishiriki piya katika matangazo ya kawaida ya habari ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC.
Wenzake katika Idhaa ya Kiswahili ya BBC wanamkumbuka Fred kuwa mtu mwema, mpole, mchangamfu na aliyepatana na wote. Alikuwa mtangazaji mtulivu na akishikilia kazi alihakikisha anaimaliza vema.
Alishiriki katika vipindi muhimu na vilivyopata sifa hasa vya sanaa, utamaduni na jamii kutokana na kuwafahamu wakaazi wengi wa London hasa wenye asili ya Afrika Mashariki.
Fred atakumbukwa kwa umahiri wake katika matangazo ya kawaida ya habari ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC.
Shukran za dhati kwa Shirika la BBC kwa kushughulikia na kugharamia mipango yote ya kuusafirisha mwili wa marehemu Fred hadi Tanzania.
Pia shukran kwa wote walioshiriki kwa namna moja ama nyingine kufanikisha mipango ya yote kuhusu msiba huu. Imetolewa na:
Zawadi Machibya
Mratibu wa Mazishi
Idhaa ya Kiswahili ya BBC
London
Kwa maelezo zaidi piga simu
+44 795 260 7038

Tuesday, December 11, 2012

WHAT IS SAFE HARBOR AND MEDIA NETWORK?


  1. It is faith and community based organization operating from Tanzania, to the international community. By faith, it is an extension of Christ Ministry to reach, people with message of the love of God and His eternal
  2. By community, it is there to be a house of development, encouragement, heritage care, and hand of grace, a house of refugees and house of those who are suffering from poverty, diseases, ignorance and lack of communication.
  3. It is a network of safety for the needy and information facilitation.
  4. Safe harbor and Media Network was birthed out of the vision of its founder Casmil and Zawadi Machibya (Mr.  & Mrs.). The vision originated from the Lord (inspired through God’s grace) to operate in the community into a step of advance living standards and peace advocacy.
  5. Safe Harbor is a non-profit and non-government (NGOs), international vision.

THE REAL SITUATION.
We know many people have suffered from been abused, have missed hope and direction. The society experiences a number of difficulties and misses a safe palce to lean. People’s purpose and functions are not well known others have suffered rejection and hurt because of diseases ignorance and poverty. Any do to know that they can discover where they can be safe by knowing their destiny. In this situation, thre is a very big world of needy people. Needs like heritage care for widows, old age support, street children, orphans and many more, call for a visionary and powerful people who will lead these and others to a safe harbor.

Information is power. A number of people today need quit proper information at the right time. Information make people know where they came from, where they ae and where they are going. Media network, stronger and operational is also needed. Local people normally miss this great opportunity.


Mr. and Mrs. Machibya


VISION
  1. Genuine “Visionary People” are people with vision from God.
  2. The vision of safe Harbor and Media Network is to produce a community of balanced, developed (independent) and problem overcoming people.  A people of human interpretation and understanding; people of human of courage with zeal according to knowledge.
  3. Safe Harbor and Media Network is the voice of the people who have availed to be corporate expression and testimony in the earth.


    Zawadi Machibya in the field.
  4. The vision will be achieved through information, counseling guidance, furnishing resources for nurturing and accountability, role playing, prayer, drama, music concert, sports, games and media. (Electronic and print media)
  5. The vision also will be revealed more fully daily in development and knowing the plan of God.

MISSION
  1. is to mobilize people to respond to the mandate of development.
  2. We endeavor to reach unexplored areas and to unreached people in our country, in the 3rd world countries and international community.
  3. By unified effort, the organization will cross every social, denominational, cultural, traditional, tribal, religious background with solution message.
  4. We envision Safe Harbor and Media Network to be a place of safe of both men and women, youth and children. All receive healings, deliverance, support, helps and accountability.
  5. Our commitment is to serve and help people worldwide to experience developments

The great thing in our mission is not so much where we are but in which direction we are moving.


PURPOSE AND OBJECTIVES:
In order to accomplish our mission, we will pursue for primary purpose and objectives to server and help people as follows
  • To establish and provide centre for street children, education, orphanange, health, recreation, old age support, moral charity and environmental activities
  • To reach local and unreached  areas with the development programs/projects
  • To help or establish dynamic growing local projects building on development foundations.
  • To help people individually as well as groups to state various development projects that sustain and help to lift up their standards of living.To touch lives in every level of their existence: their social life, their family life, and their financial and physical needs

    Zawadi Machibya in the field.
  • To open education institutes and schools of various courses
  • To touch lives in every level of their existence: their social life, their family life, and their financial and physical needs.
    Mrs. Zawadi Machibya in a teaching ministry at Morogoro, Tanzania
  • Provides training programmes in many areas of educational.  Provide both short and long terms education.
  • Provide a basis for nurturing and accountability and provide hand ministry and helps.
  • To establish services in mass communications through mass media, journalism, broadcasting, communication systems, public relations, designs, graphics, posters, internet, printing, production, advertisement and much more.
  •  To cooperate with other NGOs, societies, organizations, mission, ministries, and the like within and outside the country.
  • To establish and oversee NGOs that become affiliated with SAFE HARBOR AND MEDIA NETWORK, particularly to help the effected and left destitute by HIV/AIDS epidemic as well as parental misconduct in rearing in order to help the community.

BACKGROUND


  1. Zawadi Machibya is a wife to Rev. Casmil Machibya. They have  their children named Milton, Gift and Godson. These are the founders and leaders of S.H.M. Network and sister ministry W.C.P.M (World Changers Prophetic Missions).
  2. Zawadi Machibya has been working with Radio Tanzania and state Television (Tanzania Broadcasting Services) as a senior broadcast journalist since 1994. She is also the President and Chief Executive Officer (CEO) of Safe Harbor and Media Network (Organization).
Zawadi and her team willingly welcome you to safe  harbor and Media Network East Africa
Mr. and Mrs. Machibya
  1. She has diploma in Journalism (TSJ-DSM), Certificate and diploma course in TV Broadcasting (Howard University Communication Department- USA). Soon to complete B.A. in Mass Communication at St. Augustine University of Tanzania.
  1. Zawadi and Casmil originally established the organization in obedience to God’s guidance, community co-operation and direction.
  2. Zawadi and Casmil (Mr. and Mrs.) are multi - gifted with talents on how to help others achieve freedom, deliverance and understanding of development destinies.
  3. Zawadi and her team willingly welcome you to safe  harbor and Media Network East Africa

POSTED STORIES

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...